PASTOR MYAMBA FILMS

Friday, June 29, 2012

QUEEN SPEAR NI BALAA

 Hii ni Poster ya Queen Spear,iliyosheheni mastaa kibao..inatabiliwa kuwa ni filamu itakayofanya vizuri sana katika soko la filamu Tanzania..Usikose kununua inaingia madukani sio mda mrefu. Queen Spear itasambazwa na kampuni ya Bornagain Films Production..imeshootiwa na Sophia Records.



 Jackline Pentezel ambae ameonyesha uwezo wa hali ya juu sana kuibeba movie hii ya Queen Spear..



 Katika set ya shooting ya movie ya Queen Spear.



Tuesday, December 27, 2011

JE TUNATENGENEZA FILAMU AMBAZO WATU WANAZIHITAJI?.

''The most important quality in a filmmaker is… having a balance between creativity, understanding the tools of the trade, and having a keen business sense.''
Whereas many filmmakers have an unbridled creative passion for telling stories and know the tools of their trade, few understand how to create and package content that distributors and audiences want to see.

TANZANIA FILM TRAINING CENTER IKO TAYARI..

Tar 4 ndio siku ambapo wanafunzi wote wa Tanzania film Training center watakutana kwaajili ya photo shut!! na video interview!..baadhi ya vyombo vya habari vitarusha interview hiyo.

Monday, August 1, 2011

DOKI APANIA KUFANYA VIZURI AKIPATA NAFASI YAKUCHEZA NAMI KAMA MAMA MCHUNGAJI

Doki amepania kufanya vizuri sana endapo atapata nafasi yakucheza na mimi kwa nafasi ya mama mchungaji...amesema atanionyesha kuwa yeye ni mtu sahihi wa nafasi hiyo ya umama mchungaji na wengine wanabahatisha tuuu..hahaha karibu sana Doki ngoja nikupe hiyo nafasi katika filamu ijayo..

Wednesday, July 20, 2011

AFRICA INTERNATIONAL FILM FESTIVAL


Watanzania lazima tujitokeze kwenye Africa International Film Festival..dada yetu Monalisa kashatia timu huko katika category ya Pan Africa film actress..Basi tuwe wazalendo kwa kumpigia kura zakutosha ili ashinde..

Monday, July 11, 2011

POLE SANA SIMON MWAKIFAMBA KWA AJALI YA GARI..

Pole sana Mwakifamba Rais wetu wa Taff kwakupata ajali ya Gari juzi mitaa ya Tegeta..Mungu ni mwaminifu na hatimaye umekuwa salama..ni maombi yangu Mungu azidi kukupa nguvu,na akuponye haraka na maumivu ya hapa na pale ili ulendelee kuchapa kazi.

Sunday, July 10, 2011

WOLPER AKWEA JUKWAA BILA TAARIFA.


Msanii wa filamu Jackline Wolper aliamua kukwea jukwaa ambalo mheshimiwa Rais wa Taff Simon Mwakifamba alikuwa akihutubia mbele ya wadau wa filamu Tanzania na viongozi wengi wa serikali,Uamuzi huo wa Wolper kukwea jukwaa ulifanyika ndani ya fahamu zake pekeyake japo haukuonyeshwa katika ratiba ya siku ile,hivyo naweza nikaita ni bonge la suprise...Bado sijajua lengo binafsi la Wolper kukwea jukwani hapo,yawezekana alikuwa anakitu chakutaka kutushirikisha tuliokuwepo pale,na alizuiliwa na watu wa usalama,yawezekana alifanya jambo sahihi lakini mda haukuwa sahihi na taratibu aliyotumia yawezekana haikuwa sahihi ndio maana alizuiliwa,yawezekana angatoa taarifa mapema kuwa atafanya hivyo nadhani angewekwa kwenye ratiba na angeitwa kwa heshima kubwa...
Mmmh nitarudi baadae kutoa maoni yangu binafsi.

Tuesday, May 10, 2011

HONGERA VINCENT KIGOSI (RAY)

Mda sio mrefu nimetoka kukata simu niliyokuwa nimempigia msanii maarufu wa filamu Vincent Kigosi Maarufu Ray..mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo:

Myamba  : vipi shegu?
Ray         : Poa shegu mambo yanaendaje?.
Myamba : Mambo poa
Ray         :Uko wapi sahivi Shegu?..
Myamba  :Niko home shegu.
Ray         :Leta mpya shegu
Myamba :Jipya ni hili,makava yote uliyatengeneza ila cover hili la HANDSOME WA KIJIJI uliumiza akili  na nisipokupa hongera nitakuwa sio muungwana kabisa...nimelipenda sana cover hili na HONGERA SANA.
Ray       :dah shegu nimefurahi kusikia hivyo asante sana shegu...........
              ........mazungumzo mengine yakaendelea.........

YAKUTI AKIWA NA MSANII WA NIGERIA RAMSAY

Mwandishi nguli wa script nchini Tanzani Ally Yakuti (aliyevelia tishet nyekundu) akiwa na mcheza filamu maarufu nchini Nigeria Ramsay wakiwa  location,nyuma yao anaonekana mtu kwa mbaaali bila shaka ni Steve Kanumba (Shegu)..Yakuti kwa sasa yuko mafichoni (chimbo),kwakile alichokisema kuwa ni uwingi wa kazi alionao hivyo hataonekana mtaani kwa kipindi chote mpaka atakapomaliza kazi zote za kuandika script..

Monday, May 2, 2011

JE KUFA KWA OSAMA KUTAZUIA MAANGAMIZI?..

Bado najiuliza na kiukweli sina jibu kama kufa kwa Osama kutasitisha mashambulio yakigaidi yaliyokuwa yakiendelea Dunia nzima,ama la yanawezachochea maangamizi zaidi hasa ukiangalia historia na desturi ya JIHAD..Anyway tumwachie Mungu. 

BORNAGAIN FILMS PRODUCTION YAKAMILISHA WIMBO WA KOKO WA MZEE KING KIKII

Baada ya kampuni ya BORNAGAIN FILMS PRODUCTION kufanya vizuri katika kutengeneza video ya wimbo wa mzee king kikii alioimba maalumu kwaajili ya kuipongezaTakukuru na pia kumpongeza Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Jakaya Mrisho kikwete,Sasa imekamilisha kutengeneza video ya wimbo wa koko wa mzee King kikii,ikiwa ni katika harakati zakutengeneza album nzima ya mzee King kikii..

Saturday, April 16, 2011

AKI NA UKWA WA BONGO WAPATA MWENZAO WAMRUKIA KAMA WANAJUANA VILE

It was funny!!,kwa mara ya kwanza wameonana ila walirukiana kama vile wamewahi ishi pamoja kwa mda mrefu duuu
Poz la picha hahahaha
Haya sasa nani anachukua kifaa..
hayaaaa kazana Meya unaweza shinda!!
Mmmh!! Haya
Mzee chilo sijui ndo baba mkwee i don't knw!!!


                                          
Wewe acha utundu shuka alaaah!!!
                                          

Wednesday, April 13, 2011

PHOTO SHUT KWAAJILI YA COVER LA FILAMU YA PASTOR MYAMBA TRIAL

Myamba and Monalisa






Silvee

Bornagain family
Meya

Fety
Mogan